JE, KUTOKWA NA UCHAFU WENYE MAJIMAJI UKENI WAKATI WA UJAUZTO NI JAMBO LA KAWAIDA?

Wanawake wajawazito hupatwa na msongo wa mawazo sana kwa vitu vidogo vidogo tena vya kawaida mno.  Zipo sababu mbalimbali zinazoweza kupelekea kutokwa na uchafu wenye majimaji ukeni wakati wa ujauzito. Baadhi ya sababu hizi ni za kawaida kabisa wala hazina madhara, lakini zingine zipo zinaweza kuonyesha viashiria vya hatari, nawe unapaswa uwahi kufika hospitali mara uonapo hali dalili kama hizo.

 

Image result for image of pregnant woman

 

Anapendeza kweli mama mjamzito pale tumbo linapozidi kukua, kama unavyoona hapo juu kwenye picha.

 

Zifuatazo ni baadhi ya sababu ambazo hutokana na kutokwa na uchafu wenye majimaji ukeni wakati wa ujauzito:

 

  1. Utoko Mweupe

 

 

Kwa upande mwingine naweza nikasema hivi, utoko ni kitu cha kawaida kabisa; lakini kinaweza kuwa kibaya kwa mwanamke anapokiona kinatokea wakati wa ujauzito wake.

Related image

Lakini nipende kukufahamisha kuwa, viwango vya homoni ya estrogen huongezeka sana kadiri mimba inavyozidi kukua, na hali hii husababisha huongeza mtiririko wa damu kuelekea ukeni, na matokeo yake ndio utaona uchafu wenye majimaji ukitoka ukeni.

NUKUU: Uchafu huwa ni wa kawaida kabisa tena mzito na wenye rangi nyeupe. Mara nyingi hali hii inapojitokeza kwa mama mjamzito humpa wasiwasi sana, na imani yake huja mara tu pale anapopata maelezo kutoka kwa daktari.

 

 

  1. Ute Utelezi

 

 

Jambo lingine ni hili hapa, napenda niwajulishe kina mama wajawazito kuwa, unapobeba ujauzito, mlango wa kizazi(Cervix) huvimba na kuwa mnene kwa ajili ya kutengeneza mlango au uwazi. Ikiwa kama ungebaki katika hali hiyo, basi yaweza kuwa hiyo ndio ingekuwa njia ya kupitia bakteria kwenda kwenye mji wa mimba(uterus). Lakini mwili hauwezi kuruhusu hali hiyo ijitokeze kwa kiumbe kinachkuwa tumboni.

 

Related image

NUKUU: Hivyo basi, chini ya mlango au uwazi huo hutengenezwa ute ute mwingi, nao huzuia aina ya bakteria yoyote asiweze kuingia kwenye mfuko wa uzazi(uterus).  Mwanamke anapokaribia kujifungua, uteute huondoka na hivyo husababisha kuwepo kutokwa na uchafu wenye majimaji ukeni na unaweza ukashuka mpaka mapajani mwake. Lakini hatua hii ya ujauzito, wanawake wengi wameizoea kama hali ya kutokwa na uchafu ukeni.

 

 

  1. Mkojo

 

 

 

Kadiri tumbo la mama mjamzito linavyozidi kuwa kubwa, bila shaka huleta habari mpya kwa mama au mume anayetarajia mtoto.  Naamini kila siku inapopita lazima mama akutane na miujiza mipya.

 

Tambua leo hili kuwa, tumbo linapozidi kuwa kubwa pia husababisha msukumo hasa maeneo ya kibofu cha mkojo. Mjamzito anapokohoa, au kucheka, mara nyingi vinaweza vikashuka vitu kama majimaji ukeni. Lakini cha kushangaza ni kwamba, huu huwa ni mkojo tu.

 

  1. Kujifungua Kabla Ya Muda

 

 

Uonapo uchafu wa majimaji wenye rangi ya kahawia au nyekundu wakati wa ujauzito ukitoka ukeni, unapaswa kuwa makini sana. Yawezekana ni dalili za kujifungua kabla ya muda wake, na unapaswa kukimbia hospitali mapema ili kuonana na daktari.

Related image

Unaweza ukavua nguo ya ndani ukashangaa unaona uchafu kama huo hapo kwenye nguo ya ndani

 

 

  1. Bakteria Ukeni

 

 

Bakteria ukeni huzaliana kama matokeo ya kutokuwa na uwiano sawa wa bakteria wa asili ukeni. Uonapo dalili za uchafu wa njano au ukijivu vile ukitoka ukeni tena wenye harufu mbaya kama shombo ya samaki, basi hizi ni dalili zinazoonyesha kuwa una bakteria ukeni, na unapaswa uwe na tahadhari kubwa sana ili kuweza kupata matibabu kwa ajili ya kuzuia madhara yoyote kwa kiumbe kilichomo tumbini.

Related image

Unaweza kukutana na uchafu kama huo mama mjamzito kwahiyo unapaswa uwe makini sana.

 

 

  1. Magonjwa Ya Zinaa

 

 

Utafiti unaonyesha kwamba wanawake wajawazito wanapenda kufanya tendo la ndoa mara kwa mara, sijui kama madai haya ni ya kweli au la. Lakini ni kweli kabisa kuwa wanawake wengi wajawazito hushindwa kuvumilia wanapokuwa peke yao bila mwanaume.

 

Image result for image of a pregnant woman doing sexual intercourse with her husband

NUKUU: Mwanamke mjamzito unapopatwa na maambukizi ya zinaa wakati wa ujauzito, dalili zinazokupata huwa ni kutokwa na uchafu wa njano wenye harufu mbaya ukeni.

 

 

 

Je, unahitaji huduma? Tupigie kwa namba zetu hizi: 0752389252 au 0712181626.

 

 

Arusha-Mbauda

 

 

Karibuni sana.

270 thoughts on “JE, KUTOKWA NA UCHAFU WENYE MAJIMAJI UKENI WAKATI WA UJAUZTO NI JAMBO LA KAWAIDA?

  1. Je ni jambo la kawaida haya maji yanayotoka ukeni yanaposhuka kwenye mapaja na kwenye mashavu ya ukeni kusababisha maumivu makali kama mchubuko mapaja yanapogusana na kwenye mashavu?

    1. Sio jambo la kawaida maji kushuka mapajani. Ukiona hali kama hiyo wahi kabisa hospitali kwasababu inaweza kuwa dalili ya matatizo ya ugonjwa.

        1. Je kama maji ni mengi yanatoka ukeni yanalowanisha nguo ya ndan na mepesi yanarang ya kahawia itakuwa shida nn

  2. Natokwa uchafu huo wa njano lkn haitoi harufu yyte nmepimwa hospital magonjwa ya zinaa hakuna na unakera sana sana nikitoka haja ndogo nao unatoka
    Naomba namna ya kuutibu usitoke

      1. Mimi nikipima kipimo cha mimba mstar mmoja unatokea kwa mbaliii sana na nina week mbili na siku mbili pia dalili za mimba zimepotea nn shida

  3. Mm nna ujauzito wiki 11na siku 3 lakin leo nimeona ute wa njano na kitone cha damu kidogo…ila baada hapo nilijisaidia sikuona tena huo ute tatizo nino

    1. Hapana, hizo sio dalili za tatizo la mimba kutunga nje ya tumbo la uzazi bali ni dalili za maambukizi au mabadiriko ya homoni mwilini kwa mwanamke

  4. Mm mimba ya Tatu hii lkn hii iko tofauti natoka uchafu mweupe au nitabadilisha mtoto maan mimba zng zote sitoke uchafu na wakike nimezaa 2 lkn hii natoka uchafu sana

  5. Naomba uniunge na mm kwenye ilo group mimi tatizo langu natokwa na uouchafu wa manjano na wala hauna harufu nikivua chupi naona umefanya rangi ya manjano ila haunuki ni nini tatizo b

    1. Dada namba yako tumeshaipata naomba ufungue data yako uweze kupata maelekezo namna ya kujiunga na group letu. Karibu sana

  6. Nina ujauzito wiki ya 37sasa,ninatokwa na uchafu wenye rangi ya mawingu lkn ukifika ktk chupi unaonekana wa njano,unatoa harufu hata mm mwenyewe ninakereka,na ukeshatoka ninapata kuwashwa ukeni.Naomba uniunge kwa group.0787943767

  7. Habari za asubuhi, jamani nina mimba ya miezi 2 lakini sina dalili zozote za mjamzito, je kuna tatizo lolote

          1. Dada Sauda tayari nimeshakutumia link yetu kwenye whatssap yako naomba ufungue data yako

  8. Dr nami pia ni mhanga wa kutoka uchafu wa njano na unatoa harufu ni mjamzito miezi 7 na pia nimechoma sindano za power safe lkn siponi

  9. Nna mimba ya wiki 37 lakini natokwa na maji mepesi uken na hayanuki je inaweza leta shida naomba uniunge kwa group

  10. Mie pia ni mjamzito miezi 2 leo ni cku ya pili naona majimaji ya njano ayanuki tena asubhi ndio mengi lkn mchana ayatoki naomba uniunge mimi pia muhanga 0657004400

  11. Naitwa lilly mimi ni mjamzito na ninatokwa pia na uchafu kma huo ila nawashwa sana na nikikojoa bila kunawa ndio hatari kabisa naomba unis aide

  12. Be blessed imenisaidia kweli Leo maana nilikua sielewi huo utoko, ule Ute Kama kamasi dah Asante sana naomba uniadd na Mimi 0743014344

  13. Mimi Nina mimba ya week 4 na siku sita lakini na tokwa na uchafu mwepesi kama maji na unatoa harufu mbaya 0710726070

  14. Naomba mniunge kwenye group 0769752665

    Pia nini tiba ya mama mjamzito mwenye fangasi ukeni inawwsha anajikuna na anatoka maji meupe?je nini tulitumia tubu haikumsaidia

  15. Dr naomba kuuliza nilipata ujauzito ila mimba ilitoka nikasafishwa hospital sasa hii ni wiki ya nne ndio nimeshiriki na mume wa ila juzi nimepika mimba vimetoka vimistari viwili ila wa pili uko kwa mbali sana hiv inawezekana nina mimba ila sina dalili wala maziwa hayajaja wala kuuma no 0716593022

  16. Dr naomba kuuliza nilipata ujauzito ila mimba ilitoka nikasafishwa hospital sasa hii ni wiki ya nne ndio nimeshiriki na mume wa ila juzi nimepika mimba vimetoka vimistari viwili ila wa pili uko kwa mbali sana hiv inawezekana nina mimba ila sina dalili wala maziwa hayajaja wala kuuma no 0716593022

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *