JE, UNAFAHAMU NINI KINASABABISHA TATIZO LA MAWE KWENYE KIBOFU CHA NYONGO(GALLSTONES)? JE, NINI DALILI NA MADHARA YAKE?

Kwa kawaida kibofu cha nyongo huwa kiko maeneo ya chini ya ini. Kiungo hiki chenye umbo kama  peasi huwa kina kazi ya kuhifadhi nyongo ambayo tayari imeshatengenezwa na ini, nayo hutumika kwa ajili ya kuyeyusha mafuta. Ini pamoja kibofu cha nyongo hushikamanishwa pamoja na utumbo mwembamba kupitia mrija wa nyongo.

NUKUU: Kibofu cha nyongo kinapoathirika, basi unaweza ukapatwa na uvimbe kwenye kibofu au mawe ndani ya kibofu cha nyongo ambayo kitaalamu hujulikana kama “cholelithiasis”. Mawe ya nyongo huwa ni ugonjwa wa kawaida kabisa wa kibofu cha nyongo.

 

Je, Dalili Zake Zinakuwaje?

 

Dalili za tatizo hili huwa kama ifuatavyo:

 

  • Maumivu makali sehemu ya juu ya mkono wa kulia au tumbo la kati
  • Maumivu ambayo husambaa sehemu za bega la kulia au mgongoni
  • Tumbo kuwa gumu hasa pale linapoguswa
  • Kuhisi kichefuchefu
  • Kutapika
  • Kuhisi homa

 

NUKUU: Dalili na ishara za ugonjwa huu mara nyingi hujitokeza baada ya mlo, hasa unapokuwa mkubwa au wenye mafuta.

 

 

Je, Nini Husababisha Tatizo Hili?

 

 

Mawe ya nyongo hujitokeza pale kibofu cha nyongo kinapovimba. Kuvimba kwa kibofu cha nyongo kunaweza kusababishwa na mambo yafuatayo:

 

  1. Mawe Ya Nyongo

 

 

Mara nyingi tatizo hili hutokana na vichembechembe vigumu ambavyo huendelea kuongezeka ndani ya kibofu cha nyongo. Mawe ya nyongo yanaweza kuziba mrija ambapo nyongo hupita inapokuwa ikitoka kwenye kibofu cha nyongo. Hivyo, nyongo hujaa na kusababisha uvimbe.

 

  1. Uvimbe

 

 

 

Kivimbe kinaweza kuzuia nyongo isiweze kutiririka vizuri nje ya kibofu cha nyongo, na kusababisha nyongo ijae, hali ambayo inaweza kusababisha mawe ya nyongo(cholecystitis).

 

 

  1. Kuziba Kwa Mrija Wa Nyongo

 

 

 

 

Kuchubuka kwa mrija wa nyongo kunaweza kusababisha hali ya kuziba ambayo hufanya mawe ya nyongo kuongezeka.

 

 

  1. Maambukizi

 

 

 

Ukimwi pamoja na maambukizi mbalimbali ya virusi pia yanaweza kusababisha kuvimba kwa kibofu cha nyongo.

 

 

  1. Matatizo Ya Mishipa Ya Damu

 

 

Na ieleweke kuwa, ugonjwa unapokuwa sugu unaweza kuharibu mishipa ya damu na kupunguza mbubujiko wa damu kuweza kuingia kwenye kibofu cha nyongo, hali ambayo husababisha kujengeka kwa mawe ya nyongo.

 

Je, Nini Madhara Yake?

 

Tatizo hili linapojitokeza na likadumu kwa muda mrefu bila kutibiwa  linaweza kusababisha madhara yafuatayo:

 

  • Maambukizi ndani ya kibofu cha nyongo
  • Kuharibika kwa tishu za kibofu cha nyongo
  • Kuchanika kwa kibofu cha nyongo

 

Je, Unawezaje Kujiepusha Na Tatizo Hili?

 

Unaweza kupunguza vihatarishi vya tatizo hili kwa kuchukua hatua zifuatazo:

 

  1. Kupunguza uzito taratibu
  2. Tengeneza uzito wako wa mwili uwe katika ubora wa afya
  3. Kula vyakula vizuri na pia fanya mazoezi kila siku
  4. Hakikisha unakula vyakula visivyokuwa na wingi wa mafuta na vyenye mapungu ya fiber
  5. Tumia vyakula vya matunda, mbogamboga na nafaka pia.

 

 

 

TIBA ZAKE

 

James Herbal Clinic tuna dawa za asili zenye uwezo wa kuondoa tatizo na chanzo cha mawe katika kibofu cha nyongo, nazo ni FRESH HERB, na CARD HERB.

 

Je, unahitaji huduma? Tupigie kwa namba 0752389252 au 0712181626

 

Arusha-Mbauda

 

Karibuni sana.