Ieleweke hivi, ingawa mzunguko wa hedhi wa wastani huwa siku 28, lakini unaweza kuonekana pia siku 24 au kila baada ya siku 34. Baada ya kubalehe, wanawake wengi huwa na mzunguko wa hedhi usiobadirika hata kidogo; lakini baadhi yao hubaki katika mzunguko wenye tabia ya kubadirika badirika.
NUKUU: Kutokwa damu ya hedhi kwa kawaida huwa ni siku 3-4, na wastani wa siku 5 ambao kitaalam ndio huonekana kuwa mwanamke anachukuwa muda mrefu akitokwa damu ya hedhi.
Je, Nini Visababishi Vyake?
Mzunguko wa hedhi kubadirika badirika mara nyingi husababishwa na mambo yafuatayo:
- Vichocheo kutokuwa na uwiano sawa (hormone imbalance)
- Msongo wa mawazo
- Wasiwasi
- Mazoezi mazito
- Kuporomoka kwa mimba.
- Matumizi ya madawa hasa madawa ya uzazi wa mpango, nk.
- Magonjwa sugu kama vile ya zinaa, kisukari au magonjwa ya moyo, nk
- Magonjwa katika mfumo wa uzazi hasa vivimbe kwenye vifuko vya mayai, mji wa mimba(Uterus), mirija ya mayai, kuharibika kwa ukuta wa kifuko cha uzazi, nk
Je, Dalili Zake Zinakuwaje?
Dalili za tatizo hili mara nyingi huwa kama ifuatavyo:
- Kukosa hedhi mwezi 1, 2, au 3 nk
- Maumivu ya tumbo chini ya kitovu
- Maumivu makali wakati wa hedhi
- Kutokwa na damu muda mrefu
- Kukosa hamu ya tendo la ndoa
- Sehemu ya uke kukauka ama kukosa ute
- Kutokwa na uchafu ukeni
NUKUU: Hali ya kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi huambatana na uwepo wa matatizo mengine ya uzazi, kwani damu inaweza kutoka nyingi au kidogo kidogo kwa muda mfupi au mrefu.
Je, Madhara Yake Yanakuwaje?
NUKUU: Madhara ya tatizo la hedhi kubadirikabadirika ni kupoteza uwezo wa mwanamke kupata ujauzito au kuwa mgumba.
TIBA ZAKE
James Herbal Clinic tuna tiba nzuri zenye uwezo mkubwa wa kuondoa matatizo haya ya kubadirikabadirika kwa hedhi kwa mwanamke, nazo ni CARD HERB, PHYTOGUAD na VITAMAKA.
Je, unahitaji huduma? Tupigie kwa namba hizi: 0752389252 au 0712181626
Arusha mbauda
Karibuni sana!
Je! Kuchekwa kupata hedhi kwa siku3 au kuwahi cku2 kabla ya tarehe halisi ni tatizo ???
Hapana hiyo huwa sio tatizo ni hali ya kawaida tu kwa wanawake
Je kubadirika kwa mnzunguko wa hedhi kunatatizo?? Na kushuka kila mwezi
Ukiona hivyo ujue kuwa ni tatizo kubwa tu wahi hospitali
Amen
thanks for the tips, do you have tips for maternity woman?