JE, UNAJUA CHANZO CHA KUTOKWA NA DAMU YENYE UTELEZI KAMA MAKAMASI UKENI(BLOODY MUCUS)?

 

Je, unatokwa na damu  yenye makamasikamasi au utelezi kabla ya hedhi yako na wakati mwingine ukawa na mashaka kuwa huenda kuwa ni ujauzito?

 

 

Damu yenye utelezi inapotoka kidogo maana yake ni uchafu unaotoka ukeni ukiwa na mchanganyiko na damu kutokana na hali ya ujauzito, upevushaji mayai au sababu zingine. Makala hii leo napenda nielezee visababishi vya kutokwa na damu yenye utelezi na jinsi gani inavyoweza kukutia mashaka au wasiwasi.

Je, Uchafu Wa Kawaida Unakuwaje Na Kwanini Unakuwa Wa Kahawia?

Uchafu wa kawaida unaotoka ukeni huwa umetengenezwa na aina tofauti tofauti za seli pamoja na ute kutoka kwenye shingo ya kizazi. Uchafu wa ukeni unakuwa umetengenezwa na seli aina ya epithelial, ute utokao kwenye shingo ya kizazi, bakteria wa asili wanaokuwa kwenye uke pamoja na viumbe hai wengine.

 

Kwanini Uchafu(Utoko) Wa Ukeni Unaonekana Kuwa Wa Muhimu Sana?

Uchafu utokao ukeni ni wa muhimu kwasababu unasaidia kuzuia maambukizi ukeni. Uke kwa kawaida una bakteria wa asili wajulikanao kwa jila la Lactobacillus ambao husaidia kuuweka uke katika hali ya asidi au uchachuchachu fulani. Uke unaokuwa na hali ya uchachu huzuia maambukizi kwa urahisi.

Je, Utoko Au Uchafu Wa Kawaida Unaotoka Ukeni Unakuwa Wa Rangi Gani?

 

Utoko ama uchafu unapaswa kuwa wa njano, mweupe au wa kahawia. Baadaye tutajifunza jinsi uchafu wa njano au mweupe unavyokuwa katika makala nyingine.

 

Je, Nini Kinasababisha Kutokwa Na Damu Yenye Utelezi Kama Makamasi?

Ikiwa kama una hali ya kutokwa na uchafu ukeni wenye damu kama makamasi, basi vifuatavyo hapo chini ndivyo vyanzo vya ishara unavyopaswa kuvitambua:

 

1. Ujauzito

 

Ikiwa kama una ujauzito, basi kutokwa na damu yenye utelezi kama makamasi huwa ni ishara ya awali kabisa. Hii ni kwasababu ya mgandamizo wa damu baada ya kiumbe kuanza kuumbika tumboni.

Je, Nini Maana Ya Mgandamizo Wa Damu?

 

Baada ya tendo la ndoa katika siku za hatari, huwa kuna nafasi kubwa mno ya kupata ujauzito. Ikiwa kama mbegu zitarutubisha yai, basi ndipo kiinite hutengenezwa.  Kiinitete  hubebwa na kusafirishwa kwenda kwenye kifuko cha uzazi(uterus) ambapo hupandikizwa ama kupachikwa kwenye ukuta wa mfumko wa kizazi(uterus) ambao kitaalamu hujulikana kama endometrium.

Endapo kama hali hii ya mgandamizo itatokea, basi huwa kuna kunatokea hali ya kutokwa na damu kidogo kutoka kwenye ukuta wa mfuko wa kizazi(endometrium) ambayo huchangamana na utoko au uchafu na kuwa kama damu yenye utelezi kama makamasi vile.

 

Je, Unawezaje Kutambua Kuwa Uchafu Huo Wenye Damu Yenye Utelezi Kuwa Unatokana Na Uoteshaji Ama Mpachiko Wa Kiinitete Kwenye Mfuko Wako Wa  Kizazi?

 

Damu yenye utelezi hutoka kwasababu ya hali ya mpachiko au uoteshaji (implantation) kutokea katika siku kadhaa au wiki kabla ya mzunguko wako wa hedhi. Ikiwa kama ulikuwa unapata mzunguko wa hedhi mapema sana ama kutokwa na damu kabla ya mzunguko wako wa hedhi kufika baada ya kufanya tendo la ndoa bila kutumia kinga, basi tambua kuwa hali hiyo ni ya ujauzito.

 

Je, Dalili Zingine Za Ujauzito Zikoje?

Kwa kawaida dalili zingine za ujauzito huwa kama ifuatavyo:

  • Mwili kuchoka
  • Ladha au harufu ya vyakula ama vinywaji kubadirika
  • Kuchoka kwa urahisi sana
  • Hali ya vichomi au maumivu tumboni
  • Matiti kuvimba na kuuma.

 

Je, Unaweza Kupata Wapi Vipimo Ili Kuthibitisha Kuwa Ni Ujauzito?

 

Kama una hali ya kutokwa damu yenye utelezi kama makasi vile kabla ya hedhi, basi hiyo ni ishara ya ujauzito. Kipimo cha ujauzito kinachofanyika wakati unapoona damu kidogokidogo ikitoka, chaweza kuwa hasi. Hii ni kwasababu kiwango cha kichochezi(hormone) au HCG kinachozarishwa na kondo la nyuma(placenta) baada ya kupachikwa kwa kiinitete, kitashuka sana wakati wa upachikaji(implantation).

 

Je, Nini Cha Kufanya?

Nakushauri usibiri wiki moja ipite halafu pata kipimo cha ujauzito.

2. Upevushaji Wa Yai

 

Wakati wa upevushaji, baadhi ya wanawake wanweza kupatwa na hali ya kutokwa na damu yenye utelezi kutoka ukeni mwao. Hali hii hutokana na mpasuko(rupture) wa kifuko cha yai huku kikitokwa na damu kidogo kidogo. Kutokana na upevushaji, damu hii inapochanganyikana na utoko ama uchafu wako wa ukeni, basi uchafu unakuwa wenye damu.

 

Je, Nini Maana Ya Upevushaji?

 

Upevushaji ni hali ya kuachiliwa kwa yai kutoka kwenye ovari baada ya mkomao au  mpasuko wa mfuko wa yai. Yai hili linaporutubishwa na mbegu za mwanaume hukufanya wewe mwanamke kuwa mjamzito.

 

Je, Hali Ya Upevushaji Huanzaje Na Jinsi Gani Unaweza Kuitambua?

Hali ya kutokwa na uchafu wenye damu yenye utelezi kipindi cha upevushaji hutokea majuma 2 kabla au baada ya kipindi chako cha hedhi kukoma. Dalili za kipindi cha upevushaji wa yai huwa ni kutokwa na majimaji meupe yenye kulendemka kama ute wa yai la kuku, vichomi katika tumbo la chini, kuongezeka kwa hamu ya tendo la ndoa na matiti kuuma.

 

Je, Wakati Wa Tendo La Ndoa Inakuwaje?

Hali ya tendo la ndoa inaweza kusababisha uke kuchubuka. Hali hii inaweza kusababisha kutokwa na damu ambayo huchanganyakana na uchafu wako na kuwa wa kahawia au wenye damu.

 

Je, Unaweza Kuwa Na Mashaka Kutokana Na Damu Yenye Utelezi Kukutoka Kwasababu Ya Kufanya Tendo La Ndoa?

 

La hasha! Kutokana na kufanya tendo la ndoa, damu yenye utelezi inapojitokeza hukoma ndani ya masaa au siku chache tu. Ikiwa kama utaona damu nyeusi inatoka baada ya kufanya tendo la ndoa, basi itakuwa ni dalili za uvimbe kwenye mfuko wa kizazi(uterus) kama vile Fibroids. Kwa hali hii usichelewe kabisa. Yafaa sasa ufike hospitali ili kufanya uchunguzi wa vipimo.

3. Maambukizi Katika Sehemu Za Siri Za Mwanamke

 

Je, una hali ya kutokwa na harufu mbaya ukeni? Je, unatokwa na uchafu wenye harufu mbaya? Je, unawashwa sehemu za siri pamoja na maumivu wakati wa tendo la ndoa? Uonapo hali au dalili kama hizo, basi ni rahisi sana kutokwa na damu yenye utelezi kutokana na maambukizi.

 

Maambukizi katika sehemu za uke yanaweza kusababisha kutokwa na damu ya hedhi mara mbili ndani ya mwezi. Maambukizi ambayo unaweza kuyapata ni haya:

 

  • Pangusa (Chlamydia)
  • Kisonono
  • Maambukizi ya fangasi
  • Maambukizi katika via vya uzazi au PID
  • Malengelenge(Trichomoniasis)

 

Je, Nini Cha Kufanya?

 Unapaswa ufike hospitali za wilaya au mkoa haraka sana ili kufanya uchunguzi kupitia vipimo.

4. Uzazi Wa Mpango

 

Ikiwa kama unatumia vidonge vya uzazi wa mpango au ndio umeanza kutumia dawa za kuzuia ujauzito, basi yaweza kuwa sababu ya kutokwa na uchafu wenye damu ya utelezi. Hakuna haja ya kuwa na mashaka sana kwasababu damu inayosababishwa na vidonge vya uzazi wa mpango inaweza kukoma baada ya miezi kadhaa. Hata hivyo ikiwa hali hiyo itaendelea, basi unapaswa umuone daktari wako.

5. Saratani Ya Ukuta Wa Kizazi

 

Je, una zaidi ya umri wa miaka 40 huku ukitokwa na uchafu wenye damu yenye utelezi? Basi yaweza kuwa ni kwasababu ya ugonjwa wa saratani ya ukuta wa kizazi. Na ieleweke kuwa saratani ya ukuta wa kizazi ni hali ya kuvimba  kwa ukuta wa mfuko wa kizazi. Hali hii hutokana na athari ya vichochezi vya estrogen katika ukuta wa mfuko wa kizazi.

Hali yoyote inayoendelea kwa mwanamke ya kutokwa na damu huku akiwa amefikisha umri wa kukoma hedhi(menopause), huwa ni ishara mbaya na uonapo hivyo unapaswa ufike hospitali mapema mno bila kuchelewa ili kupima saratani.

 

Sababu 9 Zinaoweza Kukutia Wasiwasi Kwanini Utokwe Na Damu Yenye Utelezi?

 

Zifuatazo ni sababu zinazoweza kukuweka katika hali ya mashaka kwanini utokwe na damu yenye utelezi:

 

  1. Damu yako inaweza kuendelea kutoka mara kwa mara huku ikiwa na utelezi
  2. Kipindi chako cha hedhi kukaa muda mrefu kuliko kawaida
  3. Kutokwa na damu nyeusi wakati wa hedhi.
  4. Kuhisi maumivu makali wakati wa hedhi
  5. Uke wako kutokwa na harufu
  6. Kuhisi hali ya muwasho sehemu za uke
  7. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa
  8. Kutokwa na damu muda mrefu ikiwa kama ulipitiliza au kushindwa kupata hedhi katika mwezi au miezi iliyopita. Hii inaweza kuwa ishara au dalili ya kuporomoka kwa mimba.
  9. Hali ya homa na kuhisi maumivu katika tumbo lako la chini.

 

Ndugu mpendwa msomaji, haya ndio maswali ambayo yamekuwa yakiulizwa na watu mbalimbali kuhusu kutokwa na uchafu wenye damu yenye utelezi. Bila shaka majibu ndio hayo hapo juu kama unavyoona.

James Herbal Clinic tunatiba za tatizo hili tena kwa uhakika. Ikiwa kama unahitaji huduma tafadhari tupigie kwa namba hizi: 0752389252 au 0712181626

 

Karibuni sana.

 

75 thoughts on “JE, UNAJUA CHANZO CHA KUTOKWA NA DAMU YENYE UTELEZI KAMA MAKAMASI UKENI(BLOODY MUCUS)?

  1. Samahani me natokwa na damu bila mpangalio ndani ya mwezi huu na pia tumbo linaniuma pamoja na maumivu nyuma ya mgongo tatizo litakua ni nini

    1. mm nipo na mimba ta mwezi mmoja lakinin natokwa na damu yenye utelezi haiwezi kuleta shidah mimba kuharibika

  2. Mm ni mjamzito wa miez mitano maji yalinitoka mengi xana xaxa hv natokwa na ute wa kuteleza uliochanganyika na damu nini tatizo….msaada plz

  3. Mm ni mjamzito wa miez mitano maji yalinitoka mengi xana xaxa hv natokwa na ute wa kuteleza uliochanganyika na damu nini tatizo….msaada plz

  4. Mm Winnie kila ikifika siku ya hatari siku 14 au 13 natokwa na damu inaanza ya makamasi alafu inakuja damu kiasi inatoka siku moja tu na kukata naomba msaada tatizo itakuwa nini

  5. me natokwa na damu bila mpangilio tena nikishamaliza kubleed baada ya siku kadhaa mbele inatoka dam nyeusi na inateleza kiasi, na pia inakuja na kukata namaanisha inaweza toka leo na kesho ikaacha ikatokaa siku inayofata, inaweza ikawaa n nini doctor

      1. Habari samahani mm huwa mwanzo damu ilikua inatoka kidoti tuuu ikaja ikaacha kama miezi mitatu ilivyokuja mwezi wa nne sasa ikaja ni kama uchafu mweusi na ni kidogo tuuu sio mwng lkn tena mwezi huuu naona tofaut chuchu zangu zimekuwa za uchungu lkn hamna dalili yeyote ya damu kutoka tafadhali unaweza kunisaidia nikajua nasumbuliwa na nn tafadhali hii hali

  6. Mim hali hii imenitokea na sijawahi patwa na hali hii hivyo kidogo nimekuwa na mashaka kuwa ni dalli za mimba je ndani ya wiki moja mimba inaweza onekana ?

  7. Natokwa na utelez wenye michiriz ya Damu mara baada tu na kamaliza hedh na ishanitokea tena ikakaamda wa majuma mawil na miez iliyofuata ikawa ya kawaida tu ila sasaivi imejirudia tena dokta nisaidie

  8. Natokwa na utelez wenye michiriz ya Damu mara baada tu ya kamaliza hedh na ishanitokea tena ikakaamda wa majuma mawil na miez iliyofuata ikawa ya kawaida tu ila sasaivi imejirudia tena dokta nisaidie

  9. Natokwa na utelez wenye michiriz ya Damu mara baada tu ya kamaliza hedh na ishanitokea tena ikakaamda wa majuma mawil na miez iliyofuata ikawa ya kawaida tu ila sasaivi imejirudia tena dokta nisaidie

  10. Mm natokwa na utelez wenye michiriz ya Damu mara baada tu ya kamaliza hedh na ilishawahi nitokea kipind flan ila ikaisha ila sasaivi imejirudia tena dokta nisaidie

  11. Samahani mm natoka damu kidogo kama juzi nilianza kuona usiku Jana imeshinda inatoka Ila kidogo sa hivi naona kidogo Kwa ndani he inaweza kuwa kuna shida.

  12. Mimi nina mimba ila ilitoka damu yenye madonge mawili sasa ni siku ya tano damu inatoka kidogo kidogo nimepima mimba bado ipo tatizo litakuwa nini

  13. samahan mm hali iyo ya kutokwa na damu yenye uterezi imeanz nitokea kwa mara ya kwanza. sijajua shida itakua nn naimba msaada plz

      1. Mm natokwa na ute mweusi wenye harufu na maumv chini ya tumbo ni baada ya mimba yangu kuharibika nini tatizo lakin pia baada ya mimba kuharibika ikapitaa miezi miwili nikatumi p2 na hali hii ikaanzaa

  14. Natokwa na damu nyepesi Kama maji,kipindi Cha hedhi ya mwanzo,halafu ni nyepesi mpk hua sijitambui Kama nableed mpk niende uwani,siku zinazofuata inabadilika tena kua nzito kidg na nyeusi tafadhali naomba msaada

  15. anayeingia period na kisha kutokwa damu nyeusi na kisha kuharisha na kutapika tatizo ni nini? ni mara ya kwanza Hali hiyo kumtokea

  16. Habari mm nina mimba ya wiki 24 natoka na uchafu wa njano kuna mda unatoka na damu nimeenda hospital wameniambia uti na Fangas wamenipa dawa lkn bado uchafu wa njano unatoka shida itakua nini

  17. Samahani Dr. Mimi nilipata ujauzito mtoto akiwa ana umri wa miezi 6 Mungu akanisaidia nikajifungua salama na sasu mdogo ana miezi tisa, sasa baada ya kujifungua nilikaa wiki 2 damu ya uzazi ikakata nikaanza kuona siku zangu kama kawaida ila ikawa ni mara 2 kwa mwezi sasa nikaenda kuweka kitanzi cha ajabu mpka sasa sielewi mpangilio wangu wa hedhi unaendaje mara itoke kidogo mara nyingi, mara siku zinapitiliza 6, mara 3 . Mara damu telezi mara nyepesi yani sielewe Dr naomba nisaidie

  18. Mimi leo nimeiona damu inateleza Sana na haitoki nyingi inatoka kidog Sana, na pia hedhi ya mwezi wa pili nilipata tareh2 ndo nikaja kuingia tena mwezi huu wa nne jana Ila hili suala la kutoka damu yenye utelezi ndo wasiwasi wangu coz hedhi zangu zote sijapata hedhi yenye damu Kama hii,samahan ndug naomba unieleweshe kea hili

  19. Habaree ,mi kabla na baada ya kumaliza hedhi natokwa na damu lakini inakua na harufu na piah nikishiriki tendo natokwa na damu inakua na harufu ya ubichi naomba msaada

  20. Habari yaani Mimi nimeingia hedhi kisha kama wiki kadhaa nkakutan kimwili lakini baada ya siku kumi natokwa na damu yenye utelezi na isiyokolea

  21. Jamani. Mm nimeona Utewenye Dani ya utelezi na tumbo kuniuma kwa mbali Ina maana ni dalili ya Mimba changa au?

  22. Samahan doctor,, mm natokwa na dam ukeni yenye asili ya kamasi n kama cku ya tano sasa cjajua tatzo ni nini

  23. Hii ni 2021, ndio napata kusoma hii mada. Baada ya kuhangaika na tatizo la kutokwa na dam yenye utelezi zaidi ya miez 2 Sasa. Miez 7 iliyopita ujauzito uliharibika nikasafishwa na kabla ya kuharibika nilipimwa na ultrasound nikaambiwa ninauvimbe pembeni ya kizazi kushoto na fibroid, Sasa nimepata mashaka sana kwasababu zinatoka lakini hazitoi harufu wala maumivu ya tumbo Sina. Naomba msaada tafadhali

  24. Habari Dr me leo ndio Mara yangu ya kwanza kutokwa na damu ya utelezi na inatoka kidogo Kama Ute vile Ila una damu, na wiki mbili zilizopita nimemaliza p.
    Pia Nina tatzo la fungus na pid nimeenda hospt nikapimwa nikpatiwa matibabu Sasa natumia Kuna micona cream natumia na dawa zingine. Je matumizi ya dawa yanaweza kuwa ndio sababu ya hyo dam dam au Nini Dr naomba unielekeze napata mawazo Sana asubuhi ya leo

    1. Pole sana dada tena sana, naomba ukapime ultrasound pia unaweza kutuma namba yako ya whatsap tukakuunganisha na darasa letu. Karibu sana

  25. Mm hii hali inanitesa sana kila nikiwa siku ya hatari ya 13 au 14 huwa natoa ute lakin kuna mda unavyotoka san huwa unatoka na damu ya utelezi na mwezi huu siku niliyotakiw kupata siku zangu nlitoka damu kidogo sana usiku na asubuh basi na mpaka leo sijapata tena siku zangu na karibia mwez unaisha sijui shida nini kwann natoka na dam ya utelez na mda mwinginr nikinywa peps pia huwa dam inatoka kidgo na kukata naomba nisaidiwe tafadhal

    1. Je, uliwahi kupima tumbo la uzazi kwa kipimo cha ultrasound? Pia unaweza kutuma namba yako ya whatsap tukakuunganisha na darasa letu

  26. Mimi nimetumia misoprostol Jana kutoa mimba ilikuwa na mwezi mmoja unaelekea miwili, lakini cha kushangaza damu inayotoka Ni kidogo bila mabonge, je kunaweza kukawa na tatizo lolote?

  27. Mim ndo nilitakiwa nione cku zang kuanzia tareh 17 lakn nimeona tareh 15 alaf ni kwa mara ya kwanza damu kutoka na utelez na ni dam nying ya period msaada tafadhal

  28. Msaada week mojs nyuma nimepima nikakuta Nina ujauzito ila nimeingia period imenipa wasiwas kupima sina mimba nin shida

  29. Mimi nina ujauzito wa week 8 na siku 4 na leo ni siku ya 6 ninapata damu sometimes vitone,sometimes damu uliiyoganda vi ponge vidogo hata vitatu lkn inakua na utelezi. Na tumbo la chini linaniuma… nilienda kupiga ultrasound wakanambia mimba haijatoka but kwenye ultrasound inaonekana ndogo kuliko umri wake hivyo wakanipa progesterone then after 2weeks nirudi kwenye ultrasound. Je is it normal reaction or ni tatizo kubwa. Na nn kisababishi

  30. Asante kwa makala hii,,mimi niliwahi kupiga ultrasound nikakutwa na ovarian cyclist sasa natokwa na damu yenye utelezi na wakati mwingine uchafu wa rangi ya brown hii hali inanitia mashaka,,siku zangu zipo kwenye mpangilio

  31. Damu yenye utelezi inapotoka siku ambazo ulitegemea kupata hedhi yaan haijachelewa imeambatana na uchafu na damu nyeusi yaweza kusababishwa na sababu mlizozitaja kwenye makala hii

  32. Mimi ni mjamzito wa wiki 5 na siku 6 lakin natokwa na matone ya dam leo siku ya tatu na nlienda spital nkaaambiwa mimba haijaharibika nirud baada ya siku tano na leo imetoka dam yenye mchanganyiko na utelez je ni dalili ya nini

  33. Naomba msaada Mimi nimemaliza period tare 22, lakini tare 3 nimeanza kutokwa na uchafu mweus na utelezi. Sijui Shid Iko wap

  34. Me nilitakiwa nipate siku zangu tareh 20 zmetoka Leo je nikawaida maana zimekuja damu kidogo na ute wenye utelezi Sasa ninawasi wasi je ni kawaida au tatizo coz natumbo linauma

  35. mm nipo na mimba ta mwezi mmoja lakinin natokwa na damu yenye utelezi haiwezi kuleta shidah mimba kuharibika

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *