Mambo 8 Yanayopelekea Mzunguko Wako Wa Hedhi Kubadirikabadirika!

Ieleweke hivi, ingawa mzunguko wa hedhi wa wastani huwa siku 28, lakini unaweza kuonekana pia siku 24 au kila baada ya siku 34. Baada ya kubalehe, wanawake wengi huwa na mzunguko wa hedhi usiobadirika hata kidogo; lakini baadhi yao hubaki katika mzunguko wenye tabia ya kubadirika badirika.

Kutokwa damu ya hedhi kwa kawaida huwa ni siku 3-4, na wastani wa siku 5 ambao kitaalam ndio huonekana kuwa mwanamke anachukuwa muda mrefu akitokwa damu ya hedhi.

Je, Nini Visababishi Vyake?

Mzunguko wa hedhi kubadirika badirika mara nyingi husababishwa na mambo yafuatayo:

  • Vichocheo kutokuwa na uwiano sawa (hormone imbalance)
  • Msongo wa mawazo
  • Wasiwasi
  • Mazoezi mazito
  • Kuporomoka kwa mimba.
  • Matumizi ya madawa hasa madawa ya uzazi wa mpango, nk.
  • Magonjwa sugu kama vile ya zinaa, kisukari au magonjwa ya moyo, nk
  • Magonjwa katika mfumo wa uzazi hasa vivimbe kwenye vifuko vya mayai, mji wa mimba(Uterus), mirija ya mayai, kuharibika kwa ukuta wa kifuko cha uzazi, nk

Je, Dalili Zake Zinakuwaje?

Kwa kawaida dalili za tatizo hili mara nyingi huwa ziko aina mbalimbali nazo huwa kama ifuatavyo:

  • Kukosa hedhi mwezi 1, 2, au 3 nk
  • Maumivu ya tumbo chini ya kitovu
  • Maumivu makali wakati wa hedhi
  • Kutokwa na damu muda mrefu
  • Kukosa hamu ya tendo la ndoa
  • Sehemu ya uke kukauka ama kukosa ute
  • Kutokwa na uchafu ukeni

NUKUU: Hali ya kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi huambatana na uwepo wa matatizo mengine ya uzazi, kwani damu inaweza kutoka nyingi au kidogo kidogo kwa muda mfupi au mrefu.

Je, Madhara Yake Yanakuwaje?

Madhara ya tatizo la hedhi kubadirikabadirika ni kupoteza uwezo wa mwanamke kupata ujauzito au kuwa mgumba kabisa.

 Je, Suluhisho Lake Ni Nini?

James & Ferdinand Herbal Clinic tuna tiba nzuri zenye uwezo mkubwa wa kuondoa matatizo haya ya kubadirikabadirika kwa hedhi kwa mwanamke. Utapata huduma, na pia kama unahitaji masomo zaidi unaweza kutuma namba yako ya WHATSAP tunakuunganisha na darasa letu.

Je, Unahitaji huduma? Basi wasiliana nasi kwa namba hizi: 0768 559 670/0712 181 626,

Arusha-Mbauda,

Karibu sana!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *